Tuesday, November 3, 2009

hii sheria vipi?Auawa Dar kwa tuhuma za wizi

Mtu mmoja anayedhaniwa kuwa ni kibaka ameuawa kwa kupigwa kwa mawe na wananchi wenye hasira kali baada ya kudaiwa kukutwa akiezua mabati katika nyumba iliyokuwa ikiendelea kujengwa.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye amesema tukio hilo limetokea jana saa 3:30 usiku Kimara Stop Over , Jijini Dar es Salaam.
Akasema marehemu akiwa na wenzake watatu walifika katika nyumba hiyo inayomilikiwa na Bathelomeo Kijazi na kuanza kuezua mabati hayo kwa lengo la kuyaiba.
Hata hivyo, akasema wakati wakiendelea na uezuaji huo, majirani walisikia na kuanza kupiga kelele zilizowashtua watu wengine na kuanza kuwafuatilia.
“Waliposikia kelele, vibaka hao waliamua kushuka huku kila mmoja akabeba bati lake na kuanza kukimbia,”akasema.
Akasema wananchi walianza kuwafukuza na kufanikiwa kumkamata kibaka mmoja.
Kamanda huyo akasema baada ya kumkamata wananchi hao walimshambulia kwa mawe ambapo jiwe moja lilimpata kisogoni na kudondoka chini.
Akasema mtu huyo alifariki dunia wakati akipelekwa Hospitali ya Mwananyamala kwa ajili ya matibabu.
Akasema katika tukio hilo vibaka hao walifanikiwa kuondoka na mabati matatu na kuongeza uchunguzi zaidi wa tukio hilo unaendelea kuwakamata vibaka waliokimbia,
mambo vipi haya?toa maoni!!!!

No comments: