Thursday, October 29, 2009

ulipuaji bomu wauwa dar

Watu wawili wamezirai baada ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) jana kufanya zoezi la kulipua mabomu katika kambi yake iliyopo Mbagala jijini Dar es Salaam.

Waliozirai katika tukio hilo la ulipuaji mabomu ni Rosemary Tarimo na aliyetambulika kwa jina la Matilda, ambao walikimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu.
Uamuzi wa Jeshi hilo kulipua mabomu yake unatokana na silaha hizo kulipuka zenyewe katika kambi ya Mbagala na kusababisha watu zaidi ya 20 katika eneo hilo kufariki dunia.
Zoezi hilo lilifanyika jana kuanzia saa 9:00 alasiri hadi saa 11:00 jioni ambapo kabla ya kufanya shughuli hiyo, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Husein Mwinyi alitoa tahadhari kwa wananchi kukaa mbali wakati ulipuaji huo ukifanyika.
Akizungumza katika tukio hilo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi alisema, licha ya taarifa kutolewa mapema kwa vyombo vya habari, ulipuaji wa mabomu hayo ulisababisha shughuli mbalimbali kusimama ikiwemo watu kufunga maduka yao na wengine kuhama nyumba kwa kuhofia kupoteza maisha yao.
Lukuvi alisema shughuli za ugawaji wa chakula katika kambi maalumu iliyojengwa kwa ajili ya kuwahifadhi watu walioathiriwa na mabomu yaliyolipuka yenyewe hivi karibuni nao ulisimama.
Aidha, Lukuvi alisema shughuli za kutathmini uharibifu wa mali uliotokana na mabomu hayo haujakamilika kutokana na ukosefu wa watalaamu kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.
Aliwaomba watu wenye ujuzi wa kufanya tathmini ya uharibifu wa mali kujitokeza haraka ili waweze kusaidia kujua thamani halisi.
Vilevile, Mkuu huyo wa mkoa alisema watu 14 bado wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na kuathiriwa na mabomu hayo yaliyolipuka huko Mbagala hivi karibuni.
Alisema mmoja wa watu hao hali yake ni mbaya na amelazwa chumba cha watu mahututi (ICU) katika hopitali hiyo.
Baada ya kutokea ajali hiyo watu mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara walianza kumimina misaada kwa wahanga ili kuwawezesha kujikimu baada ya baadhi yao kupoteza mali zao zikiwemo nyumba.
Zoezi la ilipuaji mabomu hayo jana lilishuhudiwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali, Davis Mwamunyange.
"nibudi wananchi kulindwa na majanga yanayoweza kuepukwa".

No comments: