Monday, September 28, 2009

bongo yetu shwari
katika yote ninayoyafanya hakika moyo,fikra na matumaini yangu bongo iendelee kuwa shwari,hakika bongo haina mfano pamoja na yote ambayo unaweza fanikiwa katika nchi za nje,tusiwe wachoyo wa fadhila,au vipi?

ninaamini yakuwa bongo ni kati ya nchi ambazo zina nafasi kubwa za kimaendeleo,nikweli kuwa mshiko ni haba,nikweli kuwa nchi haina uchumi ulioboreka,

haya yote ni matokeo ya ukoloni,na kamwe tusije kuutumia uchumi ulio chini kama kisingizio,wote wameanza chini lakini hawakukata tamaa na sasa wanayavuna matunda.

watanzania tulio nje tunaweza,na wala hatuna kisingizio,tuisaidie nchi yetu,tuonyeshe umoja na tuendelee kufanya kazi kwa bidii,tufaham ni kipi kimetuleta humu,tutafute namna mbalimbali zitakazo tuwezesha kushiriki katika mambo mbalimbali yanayoihusu tanzania,nafaham kuwa nivigumu sisi kupata taarifa sahihi na mwongozo,lakini kwanza tuwe wamoja,tushauriane,na tuone yale ambayo tunaweza kuyafanya,

pia ninapatikana humu http://ngasmet.topoffers.us au http://ngasmettopoffers.blogspot.com

bongo mpya ya kikwete,incredible!!!

hakika chenye mwanzo kina mwisho na siasa za kizamani hazina mpango bongo,na msela ameliona hilo,au siyo?hongera bongo tuko pamoja,soma uniambie maoni yako,tuongee bongo kama kawa.

Mheshimiwa mkubwa wa nchi,Jakaya Mrisho Kikwete,Jumatano, Sep 9, 2009, alitoka na style mpya kabisa ya kuchonga moja kwa moja na wananchi kupitia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na vyombo vingine vya utangazaji nchini kuanzia saa mbili na nusu usiku.

Mbali na TBC, televisheni nyingine za ITV, TVZ, Mlimani TV, Tumaini TV na Channel Ten zilitarajia kuonyesha mazungumzo hayo.JK alitumia aina mpya ya kuwasiliana na wananchi kwa kusikiliza hoja zao, kwa kujibu maswali , kusikiliza ushauri wao na kupata maoni juu ya mambo yanayohusu mustakabali wa bongo.

JK pia alisikiliza matarajio ya wananchi katika jitihada zao za kuboresha maisha yao kwa kujiletea maendeleo.kuanzia saa 2:30 hadi 4:00 usiku

Aidha mazungumzo hayo yalitangazwa kwenye redio
TBC-Taifa,
Sauti ya Tanzania,
Zanzibar, Radio Mlimani,
Radio Clouds,
Radio Tumaini, na
Radio Uhuru.
ushauri ulipokelewa
"hii ni kweli au jamaa anatuzuga ili apate mradi wake"

madenti hawa vipi?

Masela watatu, akiwamo denti wa kidato cha sita katika Skonga ya Sekondari ya Azania, wamenaswa wakiwafanyia (paper) mitihani wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).Frank Kaduma, aliyekuwa anamfanyia mtihani mwanafunzi aliyemtaja kwa jina moja la Tina, alikuwa ameahidiwa na mtu aliyemuunganisha na mtahiniwa huyo kuwa baada ya kutoka kwenye mtihani huo angelipwa sh 150,000.


Kwa mujibu wa Msajili wa Wanafunzi chuoni hapo,kitambulisho alichokuwa akikitumia Frank kumfanyia Tina mtihani kilikuwa na jina la Christian Mbago, mwanafunzi wa mwaka wa tatu.Akijieleza mara baada ya kunaswa Frank alisema kuwa...aliitwa na rafiki yake ambaye hata hivyo hakutaka kumtaja jina, na baadaye alimuunganisha na mtahiniwa na kukubaliana kiasi hicho cha fedha baada ya kazi hiyo kumalizika.“Mimi ninasoma Azania, nachukua PCM (Fizikia, Kemia na Hisabati), rafiki yangu anasoma masomo ya biashara na mtihani wa leo una hisabati, hivyo juzi nilikuja naye ili anionyeshe darasa na leo ndiyo nimekuja kumfanyia mtihani,” alisema Kaduma.

Wakati mwanafunzi huyo akihojiwa, mwanafunzi mwingine, John Kapinga, alikamatwa na kupelekwa katika ofisi ya msajili baada ya kukutwa akimfanyia mtihani mwanafunzi wa mwaka wa tatu chuoni hapo, Joel Mlengule, anayesoma Stashahada ya Juu ya Hifadhi ya Jamii (Advanced Diploma in Social Protection).

Kapinga, alikiri kuwa alihitimu kidato cha sita mwaka 2003, akisoma masomo ya PCM, pamoja na kuahidi kwamba angetoa ushirikiano ili kumkamata mtahiniwa halisi.“Sikutaka kufanya, ila nilishawishiwa mara nne sikutaka, hata ikafikia hatua ndugu yake kunishawishi, nikakubali, ila dhamiri ikinisuta. kwani hakuna malipo yoyote tuliyoahidiana na ndugu yangu huyo,” alisema Kapinga huku akijiinamia.Chanzo chetu kilishuhudia kitambulisho chake kikiwa na jina la Joel Mlengule, kikiwa na namba ya usajili ADSP/16492/2007 na kinamalizika muda wake mwaka huu.Kwa upande wake, Joel Mlengule, aliyefanyiwa mtihani na kukamatwa akiwa nje ya eneo la IFM akimsubiri Kapinga, alinaswa na walinzi wa chuo na kuhojiwa, ambapo alikiri kufanyiwa mtihani na Kapinga.

Mlengule ambaye ni mkazi wa Upanga, jijini Dar es Salaam, alikiri kuwapo mtu aliyemuunganisha na Kapinga, baada ya kufeli somo lake la hesabu mara mbili mfululizo, hivyo hakutaka hali hiyo imrudie, hasa ikizingatiwa kuwa huo ulikuwa mtihani wa mwisho chuoni hapo.“Ni kweli alikuwa ananifanyia mtihani baada ya kufeli somo hili mara mbili. Niliona mwaka huu, na huu ni mtihani wangu wa mwisho, mimi sijui hesabu, ndiyo maana hata aliponiambia anifundishe nilikataa na kumwomba anisaidie kunifanyia,” alisema Mlengule.

Kwa mujibu wa Msajili wa Wanafunzi chuoni hapo, tukio jingine la namna hiyo lilitokea hivi karibuni, ambapo msichana mmoja alikimbia na kuacha viatu vyake, baada ya kubainika kuwa alikuwa akimfanyia mtihani mwanafunzi ambaye jina lake halikupatikana mara moja.Aliongeza kuwa, mwaka jana matukio hayo yalitokea na imebainika kuwa kuna wakala anayewaunganisha wanafunzi wa chuo na watu wa nje kuwafanyia mitihani hiyo kinyume cha taratibu.
 
ninajiuliza tutafika kweli hivi?kwa kweli hii ni hatari kwa maendeleo ya nchi yetu,toa maoni yako by mwandishi.

bongo pia imo

tanzania ni kati ya nchi duniani zenye raslimali ya kujitosheleza,lakini ni nani anayefaidika nayo?asili mia kubwa ya rasilimali yetu bongo bado haijatumika bado na kiasi kilichogundulika,ni cha walami/wazungu,ukiuliza kwanini,utapewa sababu tele!!wewe ungelijibu vipi?




bongo inapasa kuwa na mipango endelevu ya kimaendeleo,yenye kufwatilia shughuli zote za uzalishaji,chukulia mfano madini ya tanzanite,hakika madini haya adim duniani hayana mipango madhubuti ya kitaifa,mwishowe uchimbaji holela ambao unapelekea kunufaisha nchi za nje na wananchi wao,sababu ni nini?watanzania hawana mitaji,hili ni jibu kweli?sina imani najibu hilo,mimi ninaamini,watanzania walio nje wangelishirikishwa nchi yetu ingenufaika.



kwakweli hili linasikitisha,mimi ninahofia hatima ya nchi yetu hapobaadae,na bado ninasisitiza tusiwe niwenye kujisahau na kusahau tulipotoka,tuisaidie nchi yetu,tanzania ndo sisi na sisi ndo tanzania,toa maoni ili niweze kuelewa unamawazo gani, visit http://ngasmet.topoffers.us or http://topoffers.blogspot.com for more.

Thursday, September 24, 2009

rasilimali yetu sisi wabongofrom watanzania marekani tuongee

rasilimali yetu sisi wabongofrom watanzania marekani tuongee


kilimanjaro ni kati ya milima mirefu na mashuhuri duniani,mlima huu ni kivutio kikubwa kwa watalii kutoka sehemu mbalimbali za dunia,



hizi zote zinapasa kuwa ni sababu tosha kabisa za kuulinda na kuhakikisha mlima huu unawafaidisha watanzania wote na hususan wale wa vijiji vya karibu na mlima huu wa kipekee.



ni matumaini yangu mimi na watanzania wote kuwa serekali itaendelea kuboresha sera na kanuni zinazohusian na matumizi ya mlima huu mrefu kuliko yote africa,



kwa hakika tusipoutunza kwa kuhakikisha,wapandaji hawayaaribu mazingira ya mlima,basi mlima huu wa kipekee utapoteza ubora wake na hatimae nchi itakuwa imepoteza chanzo muhimu kabisa cha mapato.



watanzania pia tunajukum la kuiunga serekali yetu mkono na kusaidia katika kuuboresha mlima huu na na mazingira yake,ili kuendelea kupata faida,na kuitumia raslimali hii kwa miaka mingi ijayo.andika maoni.