Monday, September 28, 2009

bongo mpya ya kikwete,incredible!!!

hakika chenye mwanzo kina mwisho na siasa za kizamani hazina mpango bongo,na msela ameliona hilo,au siyo?hongera bongo tuko pamoja,soma uniambie maoni yako,tuongee bongo kama kawa.

Mheshimiwa mkubwa wa nchi,Jakaya Mrisho Kikwete,Jumatano, Sep 9, 2009, alitoka na style mpya kabisa ya kuchonga moja kwa moja na wananchi kupitia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na vyombo vingine vya utangazaji nchini kuanzia saa mbili na nusu usiku.

Mbali na TBC, televisheni nyingine za ITV, TVZ, Mlimani TV, Tumaini TV na Channel Ten zilitarajia kuonyesha mazungumzo hayo.JK alitumia aina mpya ya kuwasiliana na wananchi kwa kusikiliza hoja zao, kwa kujibu maswali , kusikiliza ushauri wao na kupata maoni juu ya mambo yanayohusu mustakabali wa bongo.

JK pia alisikiliza matarajio ya wananchi katika jitihada zao za kuboresha maisha yao kwa kujiletea maendeleo.kuanzia saa 2:30 hadi 4:00 usiku

Aidha mazungumzo hayo yalitangazwa kwenye redio
TBC-Taifa,
Sauti ya Tanzania,
Zanzibar, Radio Mlimani,
Radio Clouds,
Radio Tumaini, na
Radio Uhuru.
ushauri ulipokelewa
"hii ni kweli au jamaa anatuzuga ili apate mradi wake"

No comments: