Monday, September 28, 2009

bongo yetu shwari
katika yote ninayoyafanya hakika moyo,fikra na matumaini yangu bongo iendelee kuwa shwari,hakika bongo haina mfano pamoja na yote ambayo unaweza fanikiwa katika nchi za nje,tusiwe wachoyo wa fadhila,au vipi?

ninaamini yakuwa bongo ni kati ya nchi ambazo zina nafasi kubwa za kimaendeleo,nikweli kuwa mshiko ni haba,nikweli kuwa nchi haina uchumi ulioboreka,

haya yote ni matokeo ya ukoloni,na kamwe tusije kuutumia uchumi ulio chini kama kisingizio,wote wameanza chini lakini hawakukata tamaa na sasa wanayavuna matunda.

watanzania tulio nje tunaweza,na wala hatuna kisingizio,tuisaidie nchi yetu,tuonyeshe umoja na tuendelee kufanya kazi kwa bidii,tufaham ni kipi kimetuleta humu,tutafute namna mbalimbali zitakazo tuwezesha kushiriki katika mambo mbalimbali yanayoihusu tanzania,nafaham kuwa nivigumu sisi kupata taarifa sahihi na mwongozo,lakini kwanza tuwe wamoja,tushauriane,na tuone yale ambayo tunaweza kuyafanya,

pia ninapatikana humu http://ngasmet.topoffers.us au http://ngasmettopoffers.blogspot.com

No comments: