Thursday, September 24, 2009

rasilimali yetu sisi wabongofrom watanzania marekani tuongee

rasilimali yetu sisi wabongofrom watanzania marekani tuongee


kilimanjaro ni kati ya milima mirefu na mashuhuri duniani,mlima huu ni kivutio kikubwa kwa watalii kutoka sehemu mbalimbali za dunia,



hizi zote zinapasa kuwa ni sababu tosha kabisa za kuulinda na kuhakikisha mlima huu unawafaidisha watanzania wote na hususan wale wa vijiji vya karibu na mlima huu wa kipekee.



ni matumaini yangu mimi na watanzania wote kuwa serekali itaendelea kuboresha sera na kanuni zinazohusian na matumizi ya mlima huu mrefu kuliko yote africa,



kwa hakika tusipoutunza kwa kuhakikisha,wapandaji hawayaaribu mazingira ya mlima,basi mlima huu wa kipekee utapoteza ubora wake na hatimae nchi itakuwa imepoteza chanzo muhimu kabisa cha mapato.



watanzania pia tunajukum la kuiunga serekali yetu mkono na kusaidia katika kuuboresha mlima huu na na mazingira yake,ili kuendelea kupata faida,na kuitumia raslimali hii kwa miaka mingi ijayo.andika maoni.

1 comment:

Anonymous said...

diyo lakini naamini serekali intakiwa kuilinda,au siyo? jamani kama wenzetu wanvyofanya