Thursday, October 29, 2009

ulipuaji bomu wauwa dar

Watu wawili wamezirai baada ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) jana kufanya zoezi la kulipua mabomu katika kambi yake iliyopo Mbagala jijini Dar es Salaam.

Waliozirai katika tukio hilo la ulipuaji mabomu ni Rosemary Tarimo na aliyetambulika kwa jina la Matilda, ambao walikimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu.
Uamuzi wa Jeshi hilo kulipua mabomu yake unatokana na silaha hizo kulipuka zenyewe katika kambi ya Mbagala na kusababisha watu zaidi ya 20 katika eneo hilo kufariki dunia.
Zoezi hilo lilifanyika jana kuanzia saa 9:00 alasiri hadi saa 11:00 jioni ambapo kabla ya kufanya shughuli hiyo, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Husein Mwinyi alitoa tahadhari kwa wananchi kukaa mbali wakati ulipuaji huo ukifanyika.
Akizungumza katika tukio hilo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi alisema, licha ya taarifa kutolewa mapema kwa vyombo vya habari, ulipuaji wa mabomu hayo ulisababisha shughuli mbalimbali kusimama ikiwemo watu kufunga maduka yao na wengine kuhama nyumba kwa kuhofia kupoteza maisha yao.
Lukuvi alisema shughuli za ugawaji wa chakula katika kambi maalumu iliyojengwa kwa ajili ya kuwahifadhi watu walioathiriwa na mabomu yaliyolipuka yenyewe hivi karibuni nao ulisimama.
Aidha, Lukuvi alisema shughuli za kutathmini uharibifu wa mali uliotokana na mabomu hayo haujakamilika kutokana na ukosefu wa watalaamu kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.
Aliwaomba watu wenye ujuzi wa kufanya tathmini ya uharibifu wa mali kujitokeza haraka ili waweze kusaidia kujua thamani halisi.
Vilevile, Mkuu huyo wa mkoa alisema watu 14 bado wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na kuathiriwa na mabomu hayo yaliyolipuka huko Mbagala hivi karibuni.
Alisema mmoja wa watu hao hali yake ni mbaya na amelazwa chumba cha watu mahututi (ICU) katika hopitali hiyo.
Baada ya kutokea ajali hiyo watu mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara walianza kumimina misaada kwa wahanga ili kuwawezesha kujikimu baada ya baadhi yao kupoteza mali zao zikiwemo nyumba.
Zoezi la ilipuaji mabomu hayo jana lilishuhudiwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali, Davis Mwamunyange.
"nibudi wananchi kulindwa na majanga yanayoweza kuepukwa".

Thursday, October 22, 2009

RAGE BADO YUMO!!!!! Simba wamtaka Rage kutowabeep

Wanachama wa klabu ya Simba wamemtaka Katibu Mkuu wa zamani wa Chama cha Soka Tanzaniai, FAT (sasa TFF), Ismail Aden Rage, aliyetangaza nia ya kuwania uenyekiti katika klabu hiyo 'kutowa-beep' bali agombee kweli.

Pia wanachama hao, wamesema wapo tayari kumpa nafasi hiyo Rage kutokana na wasifu wake katika soka na hususani klabu yao na hivyo wanamtaka ajitose kweli na sio kutishia toto tu.
Wakizungumza na Nipashe jana, baadhi ya wanachama hao, wakiwemo wazee walisema wamefurahishwa na taarifa kwamba Rage anataka kujitosa kwenye kinyang;anyiro cha uchaguzi mkuu ujao wa Simba, ila hawana hakika.
Mmoja wa wanachama na wazee wa klabu hiyo, Mzee Juma Hulungu, alisema kama ni kweli Rage ana nia ya kuwania uongozi Simba wanamkaribisha na kumhakikishia kuwa wanachama watampa nafasi atakayoiomba.
Hulungu, alisema hakuna wanachama wa Simba asiyemjua Rage na utendaji wake makini na jinsi alivyoisaidia mno klabu yao na hivyo ni muhimu ajitose ili wampe nafasi hiyo kuwaletea mafanikio na maendeleo.

Mwanachama mwingine 'kigogo' alisema kwa ufupi kwamba, kama ni kweli Rage anataka nafasi hiyo ajitokeze na wala asiwatie hamu wanachama kwani klabu yao inahitaji watu kama wao katika kuikwamua kimaendeleo.
Asitubeep, kama kweli anataitaka nafasi hii ajitokeze na hatutamuangusha, kwani tunathamini mchango na utendaji wake katika soka," alisema 'kigogo' huyo ambaye hakupenda kutajwa jina lake gazetini.

Rage ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Soka mkoa wa Tabora, alinukuliwa wiki iliyopita akisema ana dhamira ya kuwania Uenyekiti katika uchaguzi mkuu wa Simba utakaofanyika Desemba mwaka huu.

Kiongozi huyo anakuwa ni wa pili kutangaza kuwania nafasi hiyo, kwani tayari mwanachama mwingine wa Simba, Bossy Matola alishatangaza dhamira ya kurithi nafasi hiyo inayoshikiliwa na Hassani Dalali.

Wednesday, October 21, 2009

washa moto kikwete"wabongo tunakuaminia"

Kuna taarifa kuwa baadhi ya vigogo Serikalini wameanza kujawa hofu na kuhaha huku na huko kutokana na hofu ya kupigwa chini na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Kikwete, chanzo kikidaiwa kuwa ni fagio lake aliloanza kulipitisha kiaina katika kila eneo.

Aidha, hofu ya baadhi ya vigogo hao inadaiwa kutiwa nguvu na tetesi kuwa Rais anaendelea kuwang'oa kiujanja wale wote wanaotuhumiwa kwa makosa mbalimbali yaliyoligharimu taifa.
Hadi sasa kuna mchakato wa kuisafisha Serikali kwa kuwawajibisha wale ambao utendaji kazi wao hauridhishi na pia wale wanaokabiliwa na tuhuma mbalimbali, chanzo kimoja kutoka Serikalini kimesema.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, baada ya taarifa ya Rais kufanya mabadiliko katika safu ya Makatibu Wakuu na kuteua Mwanasheria mpya wa Serikali juzi na jana, hali imeendeea kuwa tete kwenye baadhi ya ofisi.
"Haya mabadiliko yaliyotangazwa juzi na jana yamekuwa tishio kwa baadhi ya vigogo... wengine wameanza kuhaha kutokana na hofu kuwa pengine nao watakumbwa na fagio la kuwatema kwa sababu mbalimbali," kikadai chanzo hicho.
Aidha, kikaongeza kuwa hivi sasa, baadhi ya vigogo wamekuwa hawatulii maofisini kwani muda mwingi wamekuwa wakinusanusa taarifa toka Ikulu juu ya kusikia kama kuna badiliko lolote.
Juzi, Rais Kikwete alifanya mabadiliko ya makatibu wakuu wa baadhi ya Wizara, ambapo wengine waliachia ngazi kutokana na maelezo kuwa muda wao wa kusitaafu kwa lazima umewadia ilhali wengine wakihamishwa toka wizara moja hadi nyingine.
Aidha, jana Rais Kikwete alimteua Jaji Fredirick Mwita Werema kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, akichukua nafasi ya Johnson Mwanyika ambaye anastaafu.
Hata hivyo, Mwanyika ni miongoni mwa vigogo ambao Bunge lilitaka wawajibishwe kwa tuhuma za kuhusika kwao na kashfa ya kampuni tata ya umeme ya Richmond, kama ilivyo kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Arthur Mwakapugi, ambaye naye ameondolewa nafasi hiyo na Rais kwa maelezo kuwa anakwenda likizo ya kustaafu.

Sunday, October 18, 2009

wabongo pia ni wacheshi!!!!!!!!!

Bongo kuna kina Mr Bean weengi 'Wachekeshaji' lakini kila mtu ana style yake ya uchekeshaji, huyu ye anakwambia anauwezo wa kuchekesha Ki Mr Bean vitendo bila kuongea na anaweza kwa vitendo na kulonga.
Ukipata nafasi ya kukaa na Mkwele dakika chache na kupiga naye stori unaweza kujiuliza hivi familia yake inaishi vipi naye? Si wanacheka kila saa?
Kijana huyo ana kila sifa anayotakiwa kuwa nayo mchekeshaji. Unapozungumza naye ana maneno mengi ya kuchekesha, ambayo muda wote utajikuta ukifurahi kumskiliza na kuangua kicheko.
Anaweza akakuangalia asizungumze lolote ukajikuta ukicheka tu kutokana na vitimbi vyake na jinsi anavyojibaraguza na kugeuzageuza macho na mdomo.
Mkwele ambaye ni nadhifu mno anapokuwa mitaani, anasema anaweza kuigiza vizuri zaidi vichekesho kuliko filamu.
Anasema katika filamu huwa hajisikii huru wala haoni kama anaziweza 'kufoji' au kujilazimisha. "Unajua kipaji changu mimi ni kuchekesha ndio maana mara nyingi unaniona nafanya komedi na ndio zilizoniweka kwenye chati kuliko filamu au maigizo mengine ya kawaida,"anasema.
"Komedi naimudu na naiweza kwani pamoja na kuigiza nina uwezo mkubwa wa kuitengeneza sura yangu na kuonekana kichekesho bila hata ya kuongea lolote.
"Fani ya uigizaji hasa ya komedi ni ngumu sana tofauti na watu wengine wanavyofikiria, inahitaji ubunifu wa hali ya juu ili kuikamata hadhira,"anasema Mkwele.
"Uigizaji wa kawaida pamoja na kuwa una ugumu lakini ni rahisi kwani utakapotakiwa uigize kama Baba, Hakimu, Mama mtu yeyote anaweza kufanya hivyo ilimradi awe na kipaji cha kuigiza tu.
"Lakini linapokuja suala la kuchekesha ni kipaji cha ziada usifanye masihara kubuni kitu kumfanya mtu acheke si kazi ndogo hata kidogo, ni kweli kabisa nimeshiriki katika filamu kama 'Cleopatra' na nyingine mbili lakini sioni kama ninafanya vizuri kama ninavyofanya kwenye Mizengwe."
"Unajua katika maisha, pamoja na kuwa kila mmoja wetu ana fani yake wakati mwingine si vibaya kujaribu kazi nyingine hasa katika kujitafutia riziki," anasema.
Akizungumzia wasanii anaowazimikia ndani na nje ya nchi Mkwele anasema wa ndani ni Binti Kiroboto na wasaanii wa nje ni Harrison Ford na Mr. Bean.
"Uchekeshaji kimataifa umekuwa na soko sana tofauti na hapa kwetu na hii ni kutokana na Watanzania wengi kutopenda kuthamini kazi za wenzao jambo linalotufanya tudumae.
"Lakini mipango yangu ya baadaye ni kuhakikisha kazi zangu zinafahamika kitaifa na kimataifa, si hivyo tu pia nimedhamiria kufanya kazi kwa bidii ili hadi kufikia mwaka 2012 panapo majaaliwa nianzishe kitu changu, inaweza kuwa kampuni studio au kitu chochote."anasema
Mkwele na kutoa wito kwa wasanii wote nchini waichukulia fani hiyo kama kazi na kuifanya kwa kujali miiko. "Kwa kufanya hivyo sanaa itafika mbali hata kama hatutawafikia kina Rambo lakini tutawakaribia."
"Ili ndoto za wasanii zifanikiwe serikali ina kazi kubwa ya kuwalinda wasanii kwa kutunga na kusimamia sheria zinazoangalia kazi za wasanii nchini," anasema.
Kuhusu uhusiano wa kimapenzi, Mkwele anasema ana mchumba na mtoto mmoja ingawa hakutaka kuzungumzia kiundani zaidi kwamba dada huyo ni yupi.
"Bado nazichanga ili nifunge ndoa na mchumba wangu, si unajua tena maisha yalivyoba kwa sasa?"anasema mchekeshaji huyo ambaye amekuwa kwenye chati hasa katika kikundi cha Mizengwe kinachorushwa na kituo cha televisheni ya ITV.
mambo safi bongo au siyo.hongera.

Saturday, October 17, 2009

Watanzania wawili 'waula' taasisi za kimataifa

JAJI Bernad Luanda pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Godwin Ndossia wamechaguliwa kufanya kazi katika taasisi mbili tofauti za kimataifa.


Wakati Jaji Luanda amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa chama cha majaji na mahakimu wa Jumuiya ya Madola kanda za Afrika Mashariki, Afrika ya Kati na Kusini ya Afrika, Ndossi amechaguliwa kuwa mwakilishi wa Bara la Afrika kwenye kamati ya utendaji ya Shirikisho la Kimataifa linalojishughulisha na Sayansi ya Lishe Duniani (IUNS).

Jaji Luanda alichaguliwa hivi karibuni katika uchaguzi uliofanyika katika kongamano la mkutano mkuu wa majaji ulioketi katika visiwa vya Turks na Caicos vilivyopo Caribbean.

Taarifa iliyotolewa na Msajili wa Mahakama ya Rufaa nchini, Francis Mutungi, ilisema kongamano hilo liliwachagua pia Jaji Norma Wade Miller kutoka Bermuda (Kanda ya Caribbean ) kuwa Rais wa chama hicho.

Jaji Luanda ni Rais wa chama cha majaji na mahakimu cha Tanzania, pia makamu wa kwanza wa Rais wa chama cha majaji na mahakimu cha Afrika ya Mashariki.

Ndossi yeye alichaguliwa kwenye nafasihiyo katika mkutano wa IUNS uliofanyika kuanzia Oktoba 4 hadi 9, mwaka huu nchini Thailand.

Akizungumzia jijini Dar es Salaam juzi, Ndossi alisema ni mara ya kwanza kwa Mtanzania kuteuliwa kwenye nafasi ya kuwakilisha bara la Afrika katika taasisi hiyo nyeti ya IUNS ambayo hujadili masuala muhimu ya lishe duniani.

Lakini akasema ni changamoto kubwa kwake hasa katika kipindi hiki ambacho dunia inakabiliwa na upungufu mkubwa wa chakula kutokana na mabadiliko ya tabia nchi ambayo yamesababisha ukame ambao umedumu kwa miaka miwili.

"Hali ya lishe kwa bara la Afrika ni mbaya sana. Ukame umaathiri uzalishaji wa chakula na kasi ya utapia mlo inaongezeka kwa kasi kubwa," alisema Ndossi.

Katika bara la Afrika, alisema nchi zinazokabiliwa na utapiamlo wa kutisha ni zile ambazo zinakabiliwa na machafuko ya muda mrefu ya vita kama vile Somalia na Sudan.

Utafiti uliofanywa na TFNC siku za karibuni, Ndossi alisema unaonyesha kwamba wilaya za Longodo mkoani Arusha na Nachingwea mkoani Mtwara, ndizo zilizokatika hali mbaya ya utapia mlo hapa nchini.

Katika utafiti huo ambao alisema unatarajia kutolewa na TFNC karibuni, wilaya nyingine ambazo nazo zinakabiliwa na tatizo hilo nchini pamoja na mikoa ilipo kwenye mabano ni Bagamoyo (Pwani), Same (Kilimanjaro), Ruangwa (Lindi), Kongwa (Dodoma), Monduli (Arusha) na Mufindi (Iringa).

Akielezea juu ya hali hiyo ya utapia mlo, Ndossi alisema wanawake na watoto ndio wanataabika kwa kiwango kikubwa na tatizo hilo.

Kuhusu vigezo vilivyotumika katika kupima tatizo hilo alisema: "Tulichunguza hali za afya za kinamama na watoto. Katika jamii hawa ni kama pima joto ya tatizo la utapiamlo," alisema mjumbe huyo wa Afrika IUNS.

mambo si ndo hayoo!!!je wabongo mnasemaje?sema maoni yako.

Saturday, October 3, 2009

mambo ndo hayo!!!!!bongo inatasha kimataifa

tanzania imedhiri kuwa ubora si lazima teknolojia ya juu,hii ndiyo spirit ya watanzania,kamwe haturudi nyuma kwa sababu mbazo hazina ukweli,hii ndo sababu inayonifanya kujivuna,wewe vipi?proud?let me know,soma utoe maoni
Korosho za Tanzania zimeshika nafasi ya kwanza kwa ubora katika soko la Dunia katika kipindi cha mwaka jana, imefahamika.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho nchini, Athumani Muhagama katika kikao cha kupanda dira ya bei ya zao hilo kwa msimu ujao.
Alisema ubora huo ulitokana na korosho hizo kupangwa kwenye madaraja kama wakulima walivyoshauriwa na wataalamu wa kilimo hicho na masoko ili waweze kuuza kwa bei nzuri.
Mkurugenzi huyo, alisema kwa sasa wakulima hao wana changamoto ya kuendelea kuboresha kilimo hicho na kuzingatia ushauri wa wataalamu ili zao hilo lizidi kuongoza mwaka hadi mwaka kwa ubora katika soko hilo.
Akizungumzia kuhusu mwaka juzi, alisema zao hilo halikufanya vizuri katika soko hilo kutokana na wakulima kuchanganya na takataka kwa lengo la kuongeza uzito.
Akifungua mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Magalula Said Magalula, alisema uwezo mdogo wa baadhi ya viwanda nchini wa kubangulia korosho nchini ni chanzo cha wakulima kulazimika kuuza korosho ghafi nje ya nchi, imeelezwa.
Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya wakati akifungua kikao kidogo cha Bodi ya Korosho cha upangaji bei kilichofanyika Ukumbi wa Andrew Kagwa mjini hapa. Akifungua kikao hicho kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Said Meck Sadiki, Magalula, alisema licha ya kujitokeza matatizo hayo na ya kuyumba kwa soko la Dunia, uboreshaji wa kilimo cha korosho nchini ni muhimu kwa manufaa ya mkulima kwa kuuza zao hilo kwa bei nzuri na kuwa na uhakika wa soko.
Mgalula aliwaambia wajumbe wa kikao hicho kuwa kukata tamaa kwa wakulima kumesababisha mashamba mengi ya mikorosho kuachwa bila ya kusafishwa hali inayosabisha kuzaliwa magonjwa ambayo ni chimbuko la usumbufu wa zao hilo nchini.
Alisema kuwapo kwa magonjwa kwenye mikorosho kunawafanya baadhi ya wakulima ambao bado hawajakata tamaa ya kilimo hicho kutumia madawa mengi katika kukabiliana nayo.
Magalula, alisema kuwepo kwa matumizi makubwa ya madawa katika kilimo hicho kunamuongezea gharama mkulima na kumpunguzia faida na kwa mazingira hayo ndiyo yanayomlazimisha kuendelea kudai nyongeza ya bei kila mwaka.
Alisema endapo wadau wa kilimo hicho watajipanga upya kinaweza kuwa na faida kwa wote na kuongeza pato la Serikali. Katika kikao hicho wadau wamekubaliana dira ya bei iwe Sh 675 kwa korosho ya daraja la kwanza kwa kilo na Sh 580 kwa daraja la pili.
bongo inaweza,na ninaamini iko siku tutafika,hongera bongo na wakulima hawa wanaonyesha mfano,unaofaa kuigwa.toa maoni.